Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




2 Wakorintho 3:8 - Swahili Revised Union Version

8 je! Huduma ya roho haitazidi kuwa katika utukufu?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 basi, huduma ya Roho ina utukufu mkuu zaidi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 basi, huduma ya Roho ina utukufu mkuu zaidi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 basi, huduma ya Roho ina utukufu mkuu zaidi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 je, huduma ya Roho wa Mungu haitakuwa na utukufu zaidi?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 je, huduma ya Roho haitakuwa na utukufu zaidi?

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

8 je! Huduma ya roho haitazidi kuwa katika utukufu?

Tazama sura Nakili




2 Wakorintho 3:8
24 Marejeleo ya Msalaba  

Na Roho ya BWANA itakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA;


Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa;


Tena kuhusu habari zangu, hili ndilo agano langu nao, asema BWANA; roho yangu iliyo juu yako, na maneno yangu niliyoyatia kinywani mwako, hayataondoka kinywani mwako, wala kinywani mwa wana wako, wala kinywani mwa wajukuu wako, asema BWANA, tangu leo na hata milele.


Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.


Na neno hilo alilisema kuhusu Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.


Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?


Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au Injili nyingine msiyoikubali, mnavumiliana naye punde!


Basi “Bwana” ndiye Roho; lakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru.


Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha.


Basi, ikiwa huduma ya mauti, iliyoandikwa na kuchorwa katika mawe, ilikuja katika utukufu, hata Waisraeli hawakuweza kuukazia macho uso wa Musa, kwa sababu ya utukufu wa uso wake; nao ni utukufu uliokuwa ukibatilika;


Kwa maana ikiwa huduma ya adhabu ina utukufu, seuze huduma ya haki ina utukufu unaozidi.


ili kwamba baraka ya Abrahamu iwafikie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.


Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.


Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kumkaribia Baba katika Roho mmoja.


Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, ndugu mliopendwa na Bwana, kwa kuwa Mungu amewachagua tangu mwanzo mpate wokovu, katika kutakaswa na Roho, na kuiamini kweli;


kama vile Mungu Baba alivyotangulia kuwajua katika kutakaswa na Roho, hata mkapata kutii na kunyunyiziwa damu ya Yesu Kristo. Neema na amani na ziongezwe kwenu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo