Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




2 Samueli 5:7 - Swahili Revised Union Version

7 Lakini Daudi aliiteka ngome ya Sayuni; huu ndio mji wa Daudi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Hata hivyo, mfalme Daudi aliiteka ngome ya Siyoni, yaani mji wa Daudi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Hata hivyo, mfalme Daudi aliiteka ngome ya Siyoni, yaani mji wa Daudi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Hata hivyo, mfalme Daudi aliiteka ngome ya Siyoni, yaani mji wa Daudi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

7 Lakini Daudi aliiteka ngome ya Sayuni; huu ndio mji wa Daudi.

Tazama sura Nakili




2 Samueli 5:7
27 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Daudi alisema siku hiyo, Yeye atakayewapiga Wayebusi, na apande kwenye mfereji wa maji, na kuwapiga viwete, na hao vipofu, ambao roho yake Daudi inawachukia. Kwa sababu hii watu husema, Wako vipofu na viwete hawawezi kuingia nyumbani.


Basi Daudi akakaa ndani ya ngome hiyo, akaiita mji wa Daudi. Kisha Daudi akajenga toka Milo na pande za ndani.


Basi Daudi hakutaka kulileta sanduku la BWANA kwake mjini mwa Daudi; ila Daudi akalihamisha nyumbani kwa Obed-edomu, Mgiti.


Kisha mfalme Daudi akaambiwa ya kwamba, BWANA ameibariki nyumba ya Obed-edomu, na vitu vyote alivyo navyo kwa ajili ya sanduku la Mungu. Daudi akaenda, akalileta sanduku la Mungu, toka nyumba ya Obed-edomu mpaka mji wa Daudi, kwa shangwe.


Ikawa, sanduku la BWANA lilipoingia mji wa Daudi, Mikali binti Sauli, akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele za BWANA; akamdharau moyoni mwake.


Basi Daudi akalala na babaze, akazikwa mjini mwa Daudi.


Huyo Sulemani akafanya ujamaa na Farao, mfalme wa Misri, akamwoa binti yake Farao, akamleta mjini mwa Daudi, hata alipokwisha kuijenga nyumba yake, na nyumba ya BWANA, na ukuta wa kuuzunguka Yerusalemu.


Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa makabila na wakuu wa koo za wana wa Israeli, wamwendee mfalme Sulemani huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la Agano la BWANA kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni.


Lakini binti Farao akapanda toka mji wa Daudi, mpaka hiyo nyumba yake Sulemani, aliyomjengea; kisha, aliijenga Milo.


Basi Daudi akakaa ngomeni; kwa hiyo ukaitwa mji wa Daudi.


Wakamzika katika mji wa Daudi kati ya wafalme, kwa sababu ametenda mema katika Israeli, na kwa Mungu, na katika nyumba yake.


Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa kabila, wakuu wa mbari za mababa wa wana wa Israeli, huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la Agano la BWANA kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni.


Na lango la chemchemi akalijenga Shalumu, mwana wa Kolhoze, mkuu wa Mispa akalitengeneza lango la Chemchemi akalijenga na kulifunika, akasimamisha milango yake, na vyuma vyake, na makomeo yake, na huo ukuu wa birika la Shiloa karibu na bustani ya mfalme, mpaka madaraja yashukayo kutoka mji wa Daudi.


Kwa kuwa BWANA ameichagua Sayuni, Ameitamani akae ndani yake.


Nami nimemweka mfalme wangu Juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.


Tembeeni katika Sayuni, Uzungukeni mji wote, Ihesabuni minara yake,


Mungu katika majumba yake Amejijulisha kuwa ngome.


Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako, Uzijenge kuta za Yerusalemu.


BWANA ayapenda malango ya Sayuni Kuliko maskani zote za Yakobo.


Mwimbieni BWANA akaaye Sayuni, Yatangazeni kwa watu matendo yake.


Paza sauti, piga kelele, mwenyeji wa Sayuni; Maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu kati yako.


Na Mkombozi atakuja Sayuni, kwa wao wa Yakobo waachao maasi yao, asema BWANA.


Tazama, mimi niko juu yako, Ewe ukaaye bondeni, na kwenye jabali la uwandani, asema BWANA ninyi mnaosema, Ni nani atakayeshuka apigane nasi? Au, Ni nani atakayeingia katika makao yetu?


Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njooni, twende juu mlimani kwa BWANA, na nyumbani kwa Mungu wa Yakobo; naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake; kwa maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la BWANA litatoka Yerusalemu.


kama ilivyoandikwa, Tazama, naweka katika Sayuni jiwe likwazalo, na mwamba uangushao; Na kila amwaminiye hatatahayarika.


Bali ninyi mmeufikia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi,


Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu elfu mia moja na arubaini na nne pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo