Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




1 Wathesalonike 4:4 - Swahili Revised Union Version

4 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 na kila mmoja wenu ajifunze kuutawala mwili wake mwenyewe katika utakatifu na heshima,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 ili kwamba kila mmoja wenu ajifunze kuutawala mwili wake mwenyewe katika utakatifu na heshima,

Tazama sura Nakili




1 Wathesalonike 4:4
15 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa maana huyu ni chombo kiteule kwangu, alichukue Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli.


Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao.


Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.


Nasema kwa jinsi ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wa miili yenu. Kwa kuwa kama mlivyovitoa viungo vyenu vitumiwe na uchafu na uasi mpate kuasi, vivyo hivyo sasa vitoeni viungo vyenu vitumiwe na haki mpate kutakaswa.


Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? La hasha!


Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.


Lakini ikiwa hawawezi kujizuia, na waoe; maana ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa.


Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu.


Hatimaye, ndugu zangu, mambo yoyote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo ya heshima, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema; ukiwapo wema wowote, ikiwapo sifa nzuri yoyote, yatafakarini hayo.


Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.


Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; maana wao pia ni warithi wa neema ya uzima, ili maombi yenu yasizuiliwe na chochote.


Naye Daudi akamjibu kuhani, akamwambia, Hakika tumejitenga na wanawake siku hizi tatu; napo nilipotoka, vyombo vya vijana hawa vilikuwa vitakatifu, ingawa ilikuwa safari ya kawaida; basi leo je! Vyombo vyetu havitakuwa vitakatifu zaidi?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo