Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




1 Samueli 2:4 - Swahili Revised Union Version

4 Pinde zao mashujaa zimevunjika, Na hao waliojikwaa wamepata nguvu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 Pinde za wenye nguvu zimevunjika. Lakini wadhaifu wanaendelea kupata nguvu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 Pinde za wenye nguvu zimevunjika. Lakini wadhaifu wanaendelea kupata nguvu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 Pinde za wenye nguvu zimevunjika. Lakini wadhaifu wanaendelea kupata nguvu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 “Pinde za mashujaa zimevunjika, lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 “Pinde za mashujaa zimevunjika, lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

4 Pinde zao mashujaa zimevunjika, Na hao waliojikwaa wamepata nguvu.

Tazama sura Nakili




1 Samueli 2:4
16 Marejeleo ya Msalaba  

Nawe umenipa nguvu za vita, Hunitiishia chini yangu walionishambulia.


Upanga wao utaingia mioyoni mwao wenyewe, Na nyuta zao zitavunjika.


Maana mikono ya wasio haki itavunjika, Bali BWANA huwategemeza wenye haki.


Tulieni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.


Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari.


Huko ndiko alikoivunja mishale ya uta, Ngao, upanga, na zana za vita.


Watainama chini ya wafungwa tu, wataanguka chini yao waliouawa. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.


Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.


Maana mngelipiga jeshi lote la Wakaldayo wanaopigana nanyi, wakabaki kati yao watu waliojeruhiwa tu, hata hivyo wangeondoka kila mtu katika hema yake, na kuuteketeza mji huu.


Kwa maana mwenye kuangamiza amefika kwake; Naam, amefika Babeli; Na mashujaa wake wametwaliwa; Pinde zao zimevunjika kabisa; Maana BWANA ni Mungu wa kisasi; Hakika yake yeye atalipa.


Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.


Basi simameni, mkiwa mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,


Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.


Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii;


walizima nguvu za moto, waliokoka kutoka kwa makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo