Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yohana 5:42 - Swahili Revised Union Version

Lakini nimewajua ninyi ya kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini nawajua nyinyi, najua kwamba upendo kwa Mungu haumo mioyoni mwenu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini nawajua nyinyi, najua kwamba upendo kwa Mungu haumo mioyoni mwenu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini nawajua nyinyi, najua kwamba upendo kwa Mungu haumo mioyoni mwenu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

lakini mimi ninawafahamu. Ninajua kwamba hamna upendo wa Mungu mioyoni mwenu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini ninajua kwamba hamna upendo wa Mungu mioyoni mwenu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Lakini nimewajua ninyi ya kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yohana 5:42
17 Marejeleo ya Msalaba  

Akawaambia, Ninyi ndinyi mnaojidai haki mbele ya wanadamu, lakini Mungu awajua mioyo yenu; kwa kuwa lililotukuka kwa wanadamu huwa chukizo mbele za Mungu.


na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe alijua yaliyomo ndani ya mwanadamu.


Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.


Mimi siupokei utukufu kwa wanadamu.


Mimi nimekuja kwa jina la Baba yangu, wala ninyi hamnipokei; mwingine akija kwa jina lake mwenyewe, mtampokea huyo.


Mnawezaje kuamini ninyi mnaopokeana utukufu ninyi kwa ninyi, na utukufu ule utokao kwa Mungu aliye wa pekee hamwutafuti?


Yesu akawaambia, Kama Mungu angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi; kwa maana nilitoka kwa Mungu, nami nimekuja; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma.


Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; hivyo ninyi hamsikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.


Wala ninyi hamkumjua; lakini mimi namjua. Nikisema ya kwamba simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi; lakini namjua, na neno lake nilishika.


Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii.


Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.


Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo?


Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.


nami nitawaua watoto wake kwa mauti. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye fikira na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.