Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Walawi 26:3 - Swahili Revised Union Version

Mkizifuata amri zangu, na kuyashika maagizo yangu, na kuyafanya;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Kama mkifuata masharti yangu na kuzishika amri zangu,

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Kama mkifuata masharti yangu na kuzishika amri zangu,

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

“Kama mkifuata masharti yangu na kuzishika amri zangu,

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“ ‘Ikiwa mtafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii maagizo yangu,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“ ‘Ikiwa mtafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii maagizo yangu,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mkizifuata amri zangu, na kuyashika maagizo yangu, na kuyafanya;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Walawi 26:3
19 Marejeleo ya Msalaba  

bali mkinirudia mimi, na kuzishika amri zangu na kuzitenda, watu wako waliofukuzwa wajapokuwa katika pande za mwisho za mbingu, hata hivyo nitawakusanya kutoka huko, na kuwaleta mpaka mahali pale nilipopachagua ili kuliweka jina langu hapo.


Nanyi mtamtumikia BWANA, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako.


Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi;


Naye atatoa mvua juu ya mbegu zako, upate kuipanda nchi hii; na mkate wa mazao ya nchi, nayo itasitawi na kuzaa tele; katika siku hiyo ng'ombe wako watakula katika malisho mapana.


Niliyowaamuru baba zenu, siku ile nilipowatoa katika nchi ya Misri, katika tanuri ya chuma, nikisema, Itiini sauti yangu, mkafanye sawasawa na yote niwaagizayo ninyi; ndivyo mtakavyokuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu;


Na katika mwaka wa tano mtakula matunda yake, ili ipate kuwapa mavuno yake; mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.


Kwa maana itakuwako mbegu ya amani; mzabibu utatoa matunda yake, nayo ardhi itatoa mazao yake, na hizo mbingu zitatoa umande wake; nami nitawarithisha mabaki ya watu hawa vitu hivi vyote.


Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema BWANA wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.


Na itakuwa, kwa sababu mnazisikiliza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi BWANA, Mungu wako, atakutimilizia agano na rehema aliyowaapia baba zako;


Heri wazifuao nguo zao, ili wawe na haki ya kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.