Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wafilipi 4:13 - Swahili Revised Union Version

Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Naweza kuikabili kila hali kwani Kristo hunipa nguvu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Naweza kuikabili kila hali kwani Kristo hunipa nguvu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Naweza kuikabili kila hali kwani Kristo hunipa nguvu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wafilipi 4:13
12 Marejeleo ya Msalaba  

usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kulia wa haki yangu.


Mmoja ataniambia, Kwa BWANA, peke yake, iko haki na nguvu; naam, watu watamwendea yeye, na wote waliomkasirikia watatahayarika.


Akasema, Njoo. Petro akashuka katika mashua, akatembea juu ya maji, ili kumwendea Yesu.


Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni lolote mtakalo nanyi mtatendewa.


awajalieni, kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake, kufanywa imara kwa nguvu, kwa kazi ya Roho wake katika utu wa ndani.


Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.


mkiwezeshwa kwa uwezo wote, kwa kadiri ya nguvu ya utukufu wake, mpate kuwa na subira ya kila namna na uvumilivu pamoja na furaha;


Nami namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu kwa sababu aliniona kuwa mwaminifu, akaniweka katika utumishi wake;