Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Waebrania 7:7 - Swahili Revised Union Version

Wala haikanushiki kabisa kwamba mdogo hubarikiwa na mkubwa.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hakuna mashaka hata kidogo kwamba anayebariki ni mkuu kuliko yule anayebarikiwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hakuna mashaka hata kidogo kwamba anayebariki ni mkuu kuliko yule anayebarikiwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hakuna mashaka hata kidogo kwamba anayebariki ni mkuu kuliko yule anayebarikiwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wala hakuna shaka kwamba mdogo hubarikiwa na aliye mkuu kuliko yeye.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wala hakuna shaka kwamba mdogo hubarikiwa na aliye mkuu kumliko yeye.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wala haikanushiki kabisa kwamba mdogo hubarikiwa na mkubwa.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Waebrania 7:7
16 Marejeleo ya Msalaba  

Hayo yote ndiyo makabila ya Israeli kumi na mawili. Na hayo ndiyo aliyowaambia baba yao, na kuwabariki; mmoja mmoja kwa baraka zake aliwabariki.


Ndipo Daudi akarudi ili awabariki watu wa nyumbani mwake. Na Mikali, binti Sauli, akatoka nje aende kumlaki Daudi, naye akasema, Mfalme wa Israeli alikuwa mtukufu leo namna gani, akijifunua mwili wake mbele ya vijakazi vya watumishi wake, mfano wa watu baradhuli mmojawapo, ajifunuavyo mwili wake mbele ya watu, asipokuwa na haya!


Akasimama, na kuwabariki mkutano wote wa Israeli kwa sauti kuu, akasema,


Ndipo wakasimama makuhani Walawi, wakawabariki watu; ikasikiwa sauti yao, sala yao ikafika hata makao yake matakatifu, yaani, mbinguni.


Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitanena; Na nchi isikie maneno ya kinywa changu.


Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulikana kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.


Bali yeye, ambaye uzazi wake haukuhesabiwa kuwa umetoka kwa hao, alitwaa sehemu ya kumi kwa Abrahamu, akambariki yeye aliye na ile ahadi.


Na hapa wanadamu wapatikanao na kufa hutwaa sehemu ya kumi; bali huko yeye ashuhudiwaye kwamba yuko hai.