Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Waebrania 6:14 - Swahili Revised Union Version

akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mungu alisema: “Hakika nitakubariki na nitakupa wazawa wengi.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mungu alisema: “Hakika nitakubariki na nitakupa wazawa wengi.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mungu alisema: “Hakika nitakubariki na nitakupa wazawa wengi.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

akisema, “Hakika nitakubariki na kukupa wazao wengi.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

akisema, “Hakika nitakubariki na kukupa wazao wengi.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Waebrania 6:14
10 Marejeleo ya Msalaba  

Nami nitafanya agano langu nawe, nami nitakuzidishia sana.


akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema BWANA, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,


katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki lango la adui zao;


akaniambia, Mimi hapa, nitakuongezea uzao wako, na kukuzidisha, nami nitakufanya uwe kundi la mataifa; kisha nitawapa wazao wako nchi hii baada yako, iwe milki ya milele.


Watoto wao nao uliwaongeza kama nyota za mbinguni, ukawaingiza katika nchi ile, uliyowaambia baba zao kuwa wataingia kuimiliki.


Mkumbuke Abrahamu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.


Kwa maana urithi ukiwa kwa sheria, hauwi tena kwa ahadi; lakini Mungu alimkirimia Abrahamu kwa njia ya ahadi.


BWANA, Mungu wenu, amewafanya kuwa wengi, nanyi, angalieni, mmekuwa leo mfano wa nyota za mbinguni kwa wingi.


Angalieni, nimewawekea nchi mbele yenu, ingieni mkaimiliki nchi BWANA aliyowaapia baba zenu, Abrahamu, na Isaka, na Yakobo, kwamba atawapa na uzao wao baada yao.


watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka.