Ikawa aliporudisha mkono wake, tazama, ndugu yake akatoka. Akasema, Mbona umepita kwa nguvu wewe? Mambo ya nguvu na yakuandame. Kwa hiyo jina lake likaitwa Peresi
Nehemia 11:6 - Swahili Revised Union Version Wana wa Peresi wote waliokaa Yerusalemu walikuwa watu mia nne sitini na wanane, mashujaa. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Wazawa wote wa Peresi waliokaa mjini Yerusalemu walikuwa wanaume mashujaa 468. Biblia Habari Njema - BHND Wazawa wote wa Peresi waliokaa mjini Yerusalemu walikuwa wanaume mashujaa 468. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Wazawa wote wa Peresi waliokaa mjini Yerusalemu walikuwa wanaume mashujaa 468. Neno: Bibilia Takatifu Wazao wa Peresi walioishi Yerusalemu walikuwa mia nne sitini na nane (468), wanaume wenye uwezo. Neno: Maandiko Matakatifu Wazao wa Peresi walioishi Yerusalemu walikuwa 468, watu wenye uwezo. BIBLIA KISWAHILI Wana wa Peresi wote waliokaa Yerusalemu walikuwa watu mia nne sitini na wanane, mashujaa. |
Ikawa aliporudisha mkono wake, tazama, ndugu yake akatoka. Akasema, Mbona umepita kwa nguvu wewe? Mambo ya nguvu na yakuandame. Kwa hiyo jina lake likaitwa Peresi
Uthai, mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imli, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
na Maaseya, mwana wa Baruku, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, Mshelani.
Na wana wa Benyamini ndio hawa; Salu, mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseva, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya.
Na wana wa Yuda kwa jamaa zao; wa Shela, jamaa ya Washela; wa Peresi, jamaa ya Waperesi; wa Zera, jamaa ya Wazera.