Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 29:3 - Swahili Revised Union Version

Nami nitapiga kimo juu yako pande zote, nitakuhusuru kwa ngome, nami nitajenga maboma yakuzunguke.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mimi nitapanga jeshi dhidi ya Yerusalemu, nami nitauzingira na kuushambulia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mimi nitapanga jeshi dhidi ya Yerusalemu, nami nitauzingira na kuushambulia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mimi nitapanga jeshi dhidi ya Yerusalemu, nami nitauzingira na kuushambulia.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kujenga ngome yakukuzingira.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nami nitapiga kimo juu yako pande zote, nitakuhusuru kwa ngome, nami nitajenga maboma yakuzunguke.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 29:3
9 Marejeleo ya Msalaba  

Mfalme wa Ashuru akawatuma jemadari wake, na mkuu wa matowashi, na kamanda wake, toka Lakishi, kwa mfalme Hezekia huko Yerusalemu, pamoja na jeshi kubwa. Nao wakakwea wakafika Yerusalemu. Na walipokwisha kufika, wakaja wakasimama karibu na mfereji wa birika la juu, lililo katika njia kuu ya kuuendea Uwanda wa Dobi.


Basi BWANA asema hivi katika habari za mfalme wa Ashuru, Yeye hatauingia mji huu, wala hatapiga mshale hapa, wala hatakuja mbele yake kwa ngao, wala hatajenga boma juu yake.


Na binti Sayuni ameachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu, kama kipenu katika shamba la matango, kama mji uliohusuriwa.


Katika mkono wake wa kulia alikuwa na kura ya Yerusalemu, kuviweka vyombo vya kubomolea, kufumbua kinywa katika machinjo, kuiinua sauti kwa kupiga kelele sana, kuweka vyombo vya kubomolea juu ya malango, kufanya maboma, na kujenga ngome.


Basi yule mfalme akaghadhibika; akatuma majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.


Ila miti uijuayo si miti ya kuliwa iangamize, na kuitema; ukajenge maburuji juu ya mji ufanyao vita juu yako, hata uanguke.