Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Danieli 7:12 - Swahili Revised Union Version

Na kwa habari za wale wanyama wengine, walinyang'anywa mamlaka yao; lakini maisha yao yalidumishwa kwa wakati na majira.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wale wanyama wengine walinyanganywa mamlaka yao, lakini wao wenyewe wakaachwa waendelee kuishi kwa muda fulani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wale wanyama wengine walinyanganywa mamlaka yao, lakini wao wenyewe wakaachwa waendelee kuishi kwa muda fulani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wale wanyama wengine walinyang'anywa mamlaka yao, lakini wao wenyewe wakaachwa waendelee kuishi kwa muda fulani.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

(Wanyama wengine walikuwa wamevuliwa mamlaka yao, lakini waliruhusiwa kuishi kwa muda.)

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

(Wanyama wengine walikuwa wamevuliwa mamlaka yao, lakini waliruhusiwa kuishi kwa muda fulani.)

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Kisha nao wale nyama wengine walinyang'anywa nguvu zao za kutawala, kwani walikuwa wamekatiwa wingi wa siku zao za kuwapo, wasipite wala mwaka wala siku.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Danieli 7:12
4 Marejeleo ya Msalaba  

Nikatazama wakati huo; kwa sababu ya sauti ya yale maneno makubwa iliyoyasema ile pembe; nilitazama hata mnyama yule akauawa, mwili wake ukaharibiwa, akatolewa ateketezwe kwa moto.


Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye.


Nikamwona akimkaribia kondoo dume, akamwonea hasira kali, akampiga kondoo dume, akazivunja pembe zake mbili; na huyo kondoo dume alikuwa hana nguvu kusimama mbele yake; bali akamwangusha chini, akamkanyagakanyaga; wala hapakuwapo awezaye kumwokoa kondoo dume katika mkono wake.