Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Danieli 2:3 - Swahili Revised Union Version

Mfalme akawaambia, Nimeota ndoto, na roho yangu imefadhaika hata niijue tafsiri yake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mfalme Nebukadneza akawaambia, “Niliota ndoto, nayo inanipa wasiwasi, nami nataka nijulishwe tafsiri yake.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mfalme Nebukadneza akawaambia, “Niliota ndoto, nayo inanipa wasiwasi, nami nataka nijulishwe tafsiri yake.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mfalme Nebukadneza akawaambia, “Niliota ndoto, nayo inanipa wasiwasi, nami nataka nijulishwe tafsiri yake.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

akawaambia, “Niliota ndoto inayonisumbua, nami nataka nijue maana yake.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

akawaambia, “Niliota ndoto inayonisumbua, nami nataka nijue maana yake.”

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Wakaja, wakajipanga mbele yake mfalme. Mfalme akawaambia: Nimeota ndoto, roho yangu ikahangaika, ipate kuijua maana ya hiyo ndoto.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Danieli 2:3
5 Marejeleo ya Msalaba  

Wakamwambia, Tumeota ndoto wala hapana awezaye kuifasiri. Yusufu akawaambia, Nawaomba mniambie, kufasiri si ni kazi ya Mungu?


Farao akamwambia Yusufu, Nimeota ndoto, wala hakuna awezaye kunifasiria; nami nimesikia habari zako, ya kwamba, usikiapo ndoto, waweza kuifasiri.


Hata asubuhi roho yake ikafadhaika; akapeleka watu kuwaita waganga wote wa Misri, na watu wote wenye hekima walioko. Farao akawahadithia ndoto yake, wala hakuna aliyeweza kumfasiria Farao mambo hayo.


Hata katika mwaka wa pili wa kumiliki kwake Nebukadneza, Nebukadneza aliota ndoto; na roho yake ikafadhaika, akatokwa na usingizi.


Nikaota ndoto iliyonitia hofu; mawazo niliyokuwa nayo kitandani mwangu, na njozi za kichwa changu, zikanifadhaisha.