Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Amosi 3:5 - Swahili Revised Union Version

Je! Ndege ataanguka mtegoni juu ya nchi, mahali asipotegewa tanzi? Mtego utafyatuka juu ya nchi, bila kunasa kitu chochote?

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Je, mtego bila chambo utamnasa ndege? Je, mtego hufyatuka bila kuguswa na kitu?

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Je, mtego bila chambo utamnasa ndege? Je, mtego hufyatuka bila kuguswa na kitu?

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Je, mtego bila chambo utamnasa ndege? Je, mtego hufyatuka bila kuguswa na kitu?

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini ambapo hajategewa chambo? Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini wakati hakuna chochote cha kunasa?

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini ambapo hajategewa chambo? Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini wakati ambapo hakuna chochote cha kunasa?

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Je! Ndege ataanguka mtegoni juu ya nchi, mahali asipotegewa tanzi? Mtego utafyatuka juu ya nchi, bila kunasa kitu chochote?

Tazama sura
Tafsiri zingine



Amosi 3:5
6 Marejeleo ya Msalaba  

Wenye kiburi wamenifichia mtego na kamba; Wametandika wavu kando ya njia; Wameniwekea matanzi.


Maana mwanadamu naye hajui wakati wake; kama samaki wanaokamatwa katika nyavu mbaya, na mfano wa ndege wanaonaswa mtegoni, kadhalika wanadamu hunaswa katika wakati mbaya, unapowaangukia kwa ghafla.


Tena itakuwa, kwa kadiri nilivyowaangalia, ili kung'oa, na kubomoa, na kuangusha, na kuangamiza, na kutesa; kwa kadiri iyo hiyo nitawaangalia, ili kujenga, na kupanda, asema BWANA.


Basi BWANA anayachungulia mabaya hayo, akatuletea; maana BWANA, Mungu wetu ni mwenye haki katika kazi zake zote azitendazo; na sisi hatukuitii sauti yake.


Je! Simba atanguruma mwituni, asipokuwa na mawindo? Mwanasimba atalia pangoni mwake, ikiwa hakupata kitu?


Je! Tarumbeta itapigwa mjini, watu wasiogope? Mji utapatikana na hali mbaya, asiyoileta BWANA?