Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Wakorintho 13:9 - Swahili Revised Union Version

Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Maana ujuzi wetu si kamili, na kipaji chetu cha kutangaza neno la Mungu si kamili.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Maana ujuzi wetu si kamili, na kipaji chetu cha kutangaza neno la Mungu si kamili.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Maana ujuzi wetu si kamili, na kipaji chetu cha kutangaza neno la Mungu si kamili.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa maana tunafahamu kwa sehemu na tunatoa unabii kwa sehemu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa maana tunafahamu kwa sehemu na tunatoa unabii kwa sehemu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Wakorintho 13:9
16 Marejeleo ya Msalaba  

Tazama, hivi ni viunga tu vya njia zake; Na jinsi yalivyo madogo manong'ono tusikiayo katika habari zake! Lakini ngurumo za uweza wake ni nani awezaye kuzielewa?


Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi, Hayadirikiki, siwezi kuyafikia.


Ee BWANA, Mungu wangu, umefanya kwa wingi Miujiza yako na mawazo yako kwetu; Hakuna awezaye kufananishwa nawe; Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri, Ni mengi sana hayahesabiki.


Ni nani aliyepanda mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo kwa makonzi yake? Ni nani aliyeyafunga maji ndani ya nguo yake? Ni nani aliyefanya imara ncha zote za nchi? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwanawe, kama wajua?


Akasema, Nimekabidhiwa vyote na Baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na yeyote ambaye Mwana apenda kumfunulia.


Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake?


lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.


Maana sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.


Lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.


Mtu akidhani ya kuwa anajua neno, hajui neno lolote bado, kama impasavyo kujua.


Mimi, niliye mdogo kuliko yeye aliye mdogo wa watakatifu wote, nilipewa neema hii ya kuwahubiria Mataifa utajiri wake Kristo usiopimika;


Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini tunajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo.