Yoshua 4:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
5 akawaambia: “Mulitangulie Sanduku la Agano la Yawe, Mungu wenu, mpaka katikati ya muto Yordani. Kila mumoja wenu abebe jiwe kwenye bega lake, jiwe moja kwa ajili ya kila kabila la Israeli.
Musa akaandika maagizo yote ambayo Yawe alimupa. Kisha akaamuka asubui mapema, akajenga mazabahu chini ya mulima na kusimamisha nguzo kumi na mbili kulingana na hesabu ya makabila kumi na mbili ya Israeli.
“Musikilize enyi Waisraeli! Hivi leo mumekaribia kuvuka muto Yordani, kwenda kurizi inchi ya mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi. Miji yao ni mikubwa na ina kuta zinazofika katika mawingu.