Lakini sisi wenyewe tutatwaa silaha zetu tayari kwenda kwa vita pamoja na wandugu zetu Waisraeli, na tutakuwa kwa mustari wa mbele katika vita mpaka tuwafikishe pahali watakapokaa. Wakati huo watoto wetu watakaa kwenye miji yenye kuta, kwa kujilinda na wenyeji wa inchi hii.