Yoshua 15:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 Kutoka hapo, ulielekea kwenye mulima mpaka chemichemi za Nefutoa, mpaka kwenye miji ya mulima wa Efuroni. Hapo mupaka uligeuka na kuelekea Bala, ni kusema Kiriati-Yearimu,
Daudi aliondoka pamoja nao wote kuenda Bali-Yuda kwa kuleta Sanduku la Mungu linaloitwa kwa jina la Yawe wa majeshi, anayeikaa kwenye kiti chake cha kifalme juu ya makerubi.
Daudi akiandamana na Waisraeli wote, akaenda mpaka katika muji wa Bala, ni kusema Kiriati-Yearimu, katika inchi ya Yudea, kwa kulitwaa toka kule Sanduku la Agano linaloitwa kwa jina la Yawe anayeikaa kwenye kiti chake cha kifalme juu ya makerubi.
wakaenda kupiga kambi yao kule Kiriati-Yearimu katika inchi ya Yuda. Ndiyo maana pahali pale, upande wa magaribi wa Kiriati-Yearimu pameitwa Kambi ya Dani mpaka leo.