Yoshua 12:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Vilevile, alitawala inchi yote ya Araba, kutokea bahari ya Kineroti, upande wa mashariki, mpaka Beti-Yesimoti kwenye bahari ya Chumvi na kuendelea mpaka chini ya mulima Pisiga.
Hapo mufalme Beni-Hadadi akakubaliana na mufalme Asa, akawatuma majemadari wake na waaskari wake kwenda kuishambulia miji ya Israeli. Nao wakateka miji Iyoni, Dani, Abeli-Beti-Maka, Kineroti yote, na inchi yote ya Nafutali.
Kutoka Sefamu utaelekea kusini mpaka Ribla, upande wa mashariki wa Aini; kisha mupaka huo utakwenda chini mpaka kwenye muteremuko wa upande wa mashariki wa ziwa la Kinereti,
Upande wa magaribi, inchi yao ilienea mpaka muto Yordani. Toka ziwa Galilaya upande wa kaskazini, ukashuka mpaka kwenye bahari ya Araba, ni kusema bahari ya Chumvi, mpaka kwenye miteremuko ya Pisiga, upande wa mashariki.
na kwa wafalme waliokuwa katika milima ya upande wa kaskazini, waliokuwa Araba ambayo ilikuwa upande wa kusini wa Kineroti, kwenye mabonde na waliokuwa Nafoti-Dori katika upande wa magaribi.
Mupaka wao wa upande wa mashariki ni bahari ya Chumvi mpaka pale muto Yordani unapoingilia katika bahari. Na mupaka wao upande wa kaskazini ulipita kutokea pembe ya bahari ya Chumvi pahali ambapo muto Yordani unaingilia katika bahari.
maji yaliyokuwa yanatiririka kutoka upande wa juu yalisimama na kulundikana mpaka kule Adamu kijiji kinachokuwa karibu na muji wa Zaretani. Maji yaliyokuwa yanateremuka kwenda katika bahari ya Araba, ni kusema bahari ya Chumvi, yalitoweka kabisa, watu wakavuka mbele ya Yeriko.