Wafilipi 3:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Sitaki kusema kwamba nimekwisha kufikia mwisho au kwamba nimekwisha kuwa mukamilifu. Lakini ninakaza mwendo kusudi nipate kushinda na kupokea zawadi, kwa maana Yesu Kristo amekwisha kunipokea nikuwe wake.
Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.
Lakini Bwana akamwambia: “Kwenda tu, kwa maana nimemuchagua mutu huyu kwa kunitumikia, kusudi atangaze jina langu kwa mataifa, kwa wafalme na kwa Waisraeli.
wala nguvu za juu, wala nguvu za chini, wala kiumbe kingine chochote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu aliouonyesha kwetu kwa njia ya Kristo Yesu Bwana wetu.
Kwa maana wakati wa sasa tunaona kama mwenye kuangalia ndani ya kioo kisichoonyesha wazi, lakini wakati utakaokuja tutaona waziwazi. Kwa sasa ninajua tu mambo machache, lakini nyuma nitajua kwa utimilifu kama vile Mungu anavyonijua mimi.
Munajua hakika kuwa wale wanaofanya mashindano ya kukimbia, wote wanakimbia lakini ni mumoja tu anayepokea zawadi. Basi mukimbie hata mufikie kupokea zawadi.
Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.
Kwa maana tamaa za kimwili zinapingana na tamaa za Roho Mutakatifu. Na tamaa za Roho zinapingana na tamaa za kimwili. Hao wawili wanapingana hata munashindwa kufanya sawa vile munavyotaka.
Mbele ya kuumbwa kwa dunia, Mungu alituchagua kuwa watu wake kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watakatifu na pasipo kilema mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo, sisi watumishi wa Yesu Kristo. Tunawaandikia watu wote wa Mungu wanaoungana na Yesu Kristo, wanaoishi Filipi, pamoja na wazee wa kanisa na wasaidizi.
Sisi ndio wenye kutahiriwa kwa kweli, maana tunamwabudu Mungu kwa uongozi wa Roho wake na kujivuna kwa ajili ya Yesu Kristo. Sisi hatuweki tumaini letu katika mambo ya kimwili.
Bila shaka, ninahesabu mambo yote kuwa kihombo kwa ajili ya faida kubwa ya kujua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimekubali kupoteza vyote, nikivihesabu kuwa kama mavi, kusudi nimupate Kristo
Lakini sisi tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wandugu wapendwa wa Bwana. Kwa maana Mungu amewachagua ninyi wa kwanza kuwa watu wake kusudi mupate kuokolewa kwa kutakaswa na Roho Mutakatifu na kwa kuamini maneno ya ukweli.
Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.
Lakini ninyi mumefikia kwenye mukutano wa furaha wa wazaliwa wa kwanza wa Mungu walioandikwa majina zao katika mbingu. Mumefikia vilevile karibu na Mungu, anayekuwa mwamuzi wa watu wote na kwenye nafsi kunapokuwa roho za watu wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu.
awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.
Lakini mukisha kuteswa kwa muda kidogo, Mungu mwenye neema yote aliyewaita kusudi mupate kushiriki naye katika utukufu wake wa milele katika kuungana kwenu na Kristo, yeye mwenyewe atawakamilisha. Atawatia nguvu na kuwasimamisha imara kabisa.