Waebrania 7:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Hakuna mambo yaliyoandikwa juu ya baba ya Melkisedeki, wala mama yake, wala majina ya babu zake. Tena, habari za kuzaliwa kwake na za kufa kwake hazijulikani. Anafanana na Mwana wa Mungu kwa kuwa yeye ni kuhani kwa milele.
Na katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, wakakusanya Waisraeli wote. Waliandika majina ya wote wenye umri wa miaka makumi mbili na zaidi, kulingana na jamaa zao na ukoo zao,
Huyu Melkisedeki alikuwa mufalme wa Salemu na kuhani wa Mungu Mukubwa. Abrahamu alipokuwa akirudi toka katika vita nyuma ya kuwashinda wafalme wane, Melkisedeki alikutana naye na kumubariki,
naye Abrahamu akamupa fungu moja la kumi la vitu vyote alivyoteka. Maana ya jina la Melkisedeki, kwanza ni “Mufalme wa haki,” tena ni mufalme wa Salemu, ni kusema “Mufalme wa amani.”
Lakini huyu Melkisedeki asiyekuwa wa uzao wa Lawi, alipokea fungu moja la kumi la vitu toka kwa Abrahamu. Na zaidi ya ile akamubariki Abrahamu, ambaye Mungu alikuwa amemutolea ahadi.