Waebrania 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
4 Mungu vilevile alihakikisha ushuhuda wao kwa njia ya maajabu, ya miujiza mbalimbali, na ya vitambulisho, na kwa njia ya zawadi za Roho Mutakatifu alizowapa watu kama anavyopenda.
Mufalme Herode alisikia habari za Yesu, kwa maana jina lake lilikuwa limevuma fasi zote. Watu wamoja walisema: “Huyu ni Yoane Mubatizaji aliyefufuka! Ni kwa sababu hii amepata uwezo wa kufanya miujiza.”
Paulo na Barnaba wakakaa Ikonio kwa muda murefu. Walisema kwa uhodari kabisa, wakimutumainia Bwana. Naye aliwapa uwezo wa kufanya maajabu na vitambulisho. Na kwa njia hiyo alihakikisha kwamba ujumbe walioutangaza juu ya neema yake ulikuwa wa kweli.
Kwa hiyo, ninyi wote pamoja na Waisraeli wote mujue vizuri kwamba mutu huyu anayesimama mbele yenu akiwa muzima kabisa, ni kwa uwezo wa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, yule muliyemutundika juu ya musalaba, lakini Mungu amemufufua.