Nehemia 9:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
24 Hivyo, hao wazao wakakuja na kurizi inchi. Ulishinda Wakanana na kuwatia katika mikono yao. Watu wako waliweza kuwatendea vile walivyotaka wafalme na watu wa inchi hiyo.
“Yawe, Mungu wenu hayuko pamoja nanyi? Hajawapa amani katika pande zote? Yeye aliwatia wakaaji wa inchi hii katika mikono yangu na sasa wako chini ya Yawe na watu wake.
Ninyi mulisema kwamba watoto wenu watakamatwa mateka, lakini mimi nitawafikisha watoto wenu katika inchi muliyoizarau, kusudi waijue na ikuwe makao yao.
Basi, Yoshua aliiteka inchi yote; akawashinda wafalme wa sehemu za milima, eneo la Negebu, na sehemu za inchi ya bonde na miteremuko. Hakuacha kitu chochote chenye uzima lakini aliangamiza kila kitu kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, alivyoamuru.