Nehemia 9:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
22 Ukawapatia ushindi juu ya falme na mataifa, ukawafanyia mengi kila upande. Wakashinda inchi ya Hesiboni iliyotawaliwa na mufalme Sihoni; na tena wakashinda inchi ya Basani iliyotawaliwa na mufalme Ogi.
Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.
Maana nilipowapeleka katika ile inchi niliyoapa kuwapa, kila mara walipoona kilima kirefu au miti ya majani mengi, walianza kutoa matambiko na sadaka zao na kunichokoza. Kulekule walitoa sadaka za harufu nzuri na kutoa sadaka za kinywaji.
Alifanya hivyo kisha Yawe kumushinda mufalme Sihoni wa Waamori ambaye alikuwa anakaa katika muji wa Hesiboni, na mufalme Ogi wa Basani ambaye alikuwa anakaa katika muji wa Astaroti na Edirei.
wakiwa ngambo ya muto Yordani, katika bonde linalokuwa mbele ya Beti-Peori, katika inchi iliyokuwa ya mufalme Sihoni wa Waamori, aliyetawala kutoka katika muji wa Hesiboni, ambaye Musa na Waisraeli walimushinda walipotoka Misri.
Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli kwenye muteremuko wa Beti-Horoni, Yawe akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka mbinguni wakiwa katika njia mpaka Azeka hata waliouawa kwa mawe hayo wakakuwa wengi kuliko waliouawa kwa silaha za Waisraeli.