Nehemia 6:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
11 Lakini mimi nikajiuliza ndani ya moyo: “Mutu kama mimi ataweza kukimbia? Mutu kama mimi anahitaji kuingia katika hekalu apate kuponyesha maisha yake? Sitaingia hata kidogo katika hekalu.”
Walifanya hivyo kwa kututisha wakifikiri: “Hawataendelea na kazi, kwa hiyo, hakuna litakalotendeka.” Nikamwomba Mungu wangu nikisema: “Lakini sasa, ee Mungu, ninakuomba unipe nguvu.”
Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.
Lakini Paulo akajibu: “Kwa sababu gani munalia na kunivunja moyo? Mimi niko tayari, si kwa kufungwa tu kule Yerusalema, lakini hata kufa vilevile kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”
Naye Saulo alikuwa amekubali kwamba Stefano anastahili kuuawa. Siku ile ile kanisa lililokuwa katika Yerusalema lilianza kupata mateso makubwa. Waamini wote walisambaa katika Yudea na Samaria, isipokuwa mitume tu.
kwa sababu yeye alikuwa karibu kufa kwa ajili ya kazi ya Kristo. Alihatarisha maisha yake kwa kuja kuniletea musaada ule ambao ninyi wenyewe musingeweza kunipatia.
Kwa njia ya imani, Musa alitoka katika inchi ya Misri bila kuogopa kasirani ya mufalme. Na kama vile mutu mwenye kumwona Mungu asiyeonekana, yeye hakurudi nyuma.
Alipomwua yule Mufilistini Goliati, alihatarisha maisha yake, naye Yawe aliwapa Waisraeli ushindi mukubwa. Wewe ulipoona jambo lile ulifurahi. Kwa nini unataka kutenda zambi kwa kumwanga damu isiyokuwa na kosa kwa kumwua Daudi bila sababu?”