Nehemia 6:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
10 Nilipokwenda kwa Semaya mwana wa Delaya mujukuu wa Mehetabeli, ambaye hakuruhusiwa kutoka kwake, akaniambia: “Twende tukutane katika nyumba ya Mungu na milango yake tuifunge kwa sababu leo usiku watakuja kukuua.”
Bali-Hanani mwana wa Akibori alipokufa, Hadari akatawala pahali pake, na jina la muji wake likiwa Pau. Muke wa Akibori alikuwa Mehetabeli, binti ya Matiredi, binti ya Mezahaba.
Zaidi ya hayo, alikusanya vifaa vyote vya nyumba ya Mungu, akavikatakata vipandevipande, kisha akafunga milango ya nyumba ya Yawe na kujijengea mazabahu katika kila pembe ya Yerusalema.
Tena, wamefunga milango ya baraza, wakazimisha taa, na hawajafukiza ubani wala kutoa sadaka za kuteketeza kwa moto katika Pahali Patakatifu pa Mungu wa Israeli.
Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.
“Mufanye angalisho na manabii wa uongo; kwa maana wanakuja kwenu wakionekana kwa inje kama vile kondoo, lakini ndani, wao ni kama imbwa wakali wa pori.
Muji wote ukajaa fujo na watu wakakusanyika pale mbiombio. Wakamukamata Paulo na kumukokotea mpaka inje ya hekalu, na mara moja wakafunga milango yake.