Nehemia 3:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
31 Sehemu inayofuata, tokea kwenye nyumba ya watumishi wa hekalu na wachuuzi iliyokuwa inaelekeana na Mulango wa Gereza, karibu na chumba cha juu kwenye pembe upande wa kaskazini-mashariki ikajengwa upya na Malkiya, mufua zahabu.
Sehemu inayofuata ikiwa ni sehemu yao ya pili ikajengwa upya na Hanania mwana wa Selemia, akishirikiana na Hanuni mwana wa sita wa Zalafi. Mesulamu mwana wa Berekia, akajenga upya sehemu inayoelekeana na chumba chake.
Sehemu inayofuata, ilijengwa upya na Usieli mwana wa Harihaya, mufua zahabu. Sehemu inayofuata mpaka kwenye Ukuta Mupana ikajengwa upya na Hanania, mutengenezaji wa marasi.