Nehemia 3:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
17 Nyuma ya hao, Walawi waliendelesha ujenzi mupya wa ukuta. Sehemu inayofuata ikajengwa upya na Rehumu mwana wa Bani, na Hasabia, mutawala wa nusu ya wilaya ya Keila, akajenga upya sehemu ya upande wa wilaya yake.
Sehemu inayofuata mpaka kwenye makaburi ya Daudi, kisima na majengo ya waaskari ikajengwa upya na Nehemia mwana wa Aibuki, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Beti-Suri.
Nyuma yake, sehemu zinazofuata zikajengwa upya na wandugu zao. Sehemu inayofuata ikajengwa upya na Bawayi mwana wa Henadadi, mutawala wa nusu ya wilaya ya Keila.
Kuliwekwa daraja la Walawi; pale kulisimama Yesua, Bani, Kadimieli, Sebania, Buni, Serebia, Bani na Kenani. Wakamwomba kwa sauti kubwa Yawe, Mungu wao.