Nehemia 2:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 Nilipowafikia wakubwa wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, nikawapa barua za mufalme. Mufalme alikuwa amenituma pamoja na wakubwa wa waaskari na waaskari wapanda-farasi.
Ingekuwa haya kubwa kwangu kumwomba mufalme kundi la waaskari na waaskari wapanda-farasi wa kutulinda na waadui katika njia maana nilikuwa nimekwisha kumwambia kwamba Mungu wetu anawabariki wote wanaomutafuta, lakini anawachukia na kuwaazibu wote wanaomwacha.
Nikamujibu: “Ee mufalme, ikikupendeza, ninaomba nipewe barua kusudi nizipeleke kwa watawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati kusudi waniruhusu nipite mpaka katika inchi ya Yuda.