Nehemia 11:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
17 na Matania mwana wa Mika mwana wa Zabudi, wa uzao wa Asafu, aliyekuwa kiongozi wakati wa kuomba maombi ya shukrani. Bakubukia alikuwa musaidizi wake. Pamoja nao kulikuwa Abuda mwana wa Samua mwana wa Galali wa uzao wa Yedutuni.
Zaidi ya hayo, Daudi akaweka Walawi wamoja kwa kazi mbele ya Sanduku la Agano la Yawe, wamutukuze, wamutolee shukrani na wamusifu Yawe, Mungu wa Israeli.
Viongozi wa Walawi Hasabia, Serebia, Yesua mwana wa Kadimieli walisimama kuelekeana na wandugu zao walipangwa kwa kuimba nyimbo za kusifu na kushukuru, kufuatana na amri ya mufalme Daudi, mutu wa Mungu.
Nikawakusanya viongozi wote wa Yuda kwenye ukuta na kutenga waimbaji katika makundi mawili makubwa yaliyoimba nyimbo za shukrani wakiwa katika maandamano. Kundi moja lilielekea upande wa kuume wa ukuta mpaka kwenye Mulango wa Takataka.