Nehemia 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 Lakini mukinirudilia, mukishika amri zangu na kuzifuata hata ingawa nitakuwa nimewatawanya mbali kabisa, nitawarudisha pahali nilipochagua kuwa pahali pangu pa kuabudiwa.’
vilevile wakati ule watakapokuwa katika inchi ya waadui zao, wakikugeukia kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote, na kama wakikuomba wakielekea inchi yao ambayo uliwapatia babu zao, wakielekea muji huu ambao uliuchagua na nyumba hii ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako,
Yawe alimwambia: “Nimesikiliza wakati uliponiomba na kunisihi. Nimeitakasa nyumba hii ambayo umenijengea kusudi watu waabudu jina langu hapa milele. Nitaichunga na kuipenda wakati wote.
Mumwambie Yawe: utuokoe, ee Mungu wa wokovu wetu, utukusanye pamoja na kutuokoa kutoka kwa mataifa, tupate kulisifu jina lako takatifu, kuona utukufu juu ya sifa zako.
Mungu aliyeuchagua Yerusalema kuwa pahali pake pa kuabudiwa amwangushe mufalme au taifa lolote litakalopinga amri hii au kutaka kuiharibu nyumba hii ya Mungu inayokuwa katika Yerusalema. Ni mimi Dario niliyetoa amri hii na inapaswa kushikwa.
Naye atasimika bendera kuwaita mataifa, kuwakusanya Waisraeli waliozarauliwa, kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa, na kuwarudisha toka pembe ine za dunia.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, yule anayewakusanya Waisraeli waliosambazwa.– Zaidi ya hao niliokwisha kukusanya, nitawakusanya watu wengine wakutane nao.
Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu, maana, mimi ndimi Bwana wenu. Nitawatwaa mumoja kutoka kila muji, na wawili kutoka katika kila ukoo, niwapeleke mpaka kwenye mulima Sayuni. –Ni ujumbe wa Yawe.
Enyi mataifa, musikilize neno langu mimi Yawe, mulitangaze katika visanga vya mbali, museme hivi: Aliyemusambaza Israeli, atamukusanya, atamutunza kama muchungaji anavyotunza kondoo wake.
Nitawakusanya watu kutoka inchi zote ambako kwa hasira na kasirani na chuki yangu kubwa, niliwatawanya. Nitawarudisha tena hapa, na kuwafanya wakae salama.
Baragumu kubwa itapigwa, halafu atawatuma wamalaika wake katika pande ine za dunia, kusudi wawakusanye watu wake aliowachagua, kutoka katika dunia nzima.
Basi, pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua, apaweke jina lake, hapo munaweza kuchinja ngombe au kondoo yeyote ambaye Yawe amewajalia, kama nilivyowaamuru na munaweza kula kiasi chochote munachotaka cha nyama hiyo, kama mukiwa katika miji yenu.
Musa akaendelea kusema: “Baraka na laana hizi zote zitatimizwa. Mutafikiri juu ya mambo hayo wakati Yawe, Mungu wenu, atakuwa amewatawanya kati ya mataifa.