Muhubiri 8:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
8 Hakuna mutu anayekuwa na uwezo wa kushikilia roho yake kusudi asikufe; hakuna mutu anayekuwa na uwezo juu ya siku ya kufa. Wakati wa vita hakuna kuponyoka, na uovu hauwezi kumwokoa mwovu.
Sisi wote tutakufa. Sisi ni kama maji yaliyomwangika chini ambayo hayawezi kuzoleka. Lakini Mungu hataki Abusaloma akufe sasa au aendelee kuishi mbali naye.
Watu hao wakaenda mpaka Yordani na katika njia waliona nguo na vifaa vingine Waaramu walivyoacha walipokuwa wanakimbia. Wakarudi na kumupasha mufalme habari.
Mutu hajui saa yake itafika wakati gani. Kama vile samaki wanavyonaswa katika wavu kwa bahati mbaya, na kama vile ndege wanavyonaswa katika mutego kwa rafla, ndivyo wanadamu wanavyonaswa na hasara inapowaangukia bila kutazamia.
Ninyi munajidai mumefanya agano na kifo mumefanya mapatano na kuzimu! Ninyi munasema kwamba hasara itakapokuja haitawapata, kwa sababu mumefanya uongo kuwa tegemeo lenu, na udanganyifu kuwa kikingio chenu!
Ulijiona salama katika uovu wako; ukajisemesha: Hakuna mutu anayeniona. Hekima na elimu yako vilikupotosha, ukajisemesha ndani ya moyo wako: Mimi ndiye; hakuna mwingine isipokuwa mimi.
Ni kweli Kristo alitundikwa juu ya musalaba katika hali ya uzaifu wa mwili, lakini sasa anaishi kwa uwezo wa Mungu. Nasi katika kuungana kwetu naye sisi vilevile tunakuwa zaifu. Lakini kwa ajili yenu tunaishi pamoja naye kwa nguvu ya Mungu.