Muhubiri 8:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
14 Kuna jambo moja la bure nililotambua hapa katika dunia: mara kwa mara watu wema wanatendewa jinsi waovu wanavyostahili kutendewa, nao waovu wanatendewa jinsi watu wema wanavyostahili kutendewa. Ninasema kwamba hayo nayo ni bure.
Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.
Katika maisha yangu ya bure, niliona kila kitu. Mutu wa haki anakufa ingawa ni wa haki, ambapo mutu mwovu anaendelea kuishi maisha marefu ingawa ni mwovu.
Ee Yawe, wewe ni mwenye haki, ingawa nitakushitaki. Lakini ningependa nibishane nawe juu ya mambo ya haki: Kwa nini waovu wanafanikiwa katika mambo yao? Mbona wote wanaodanganya wanastawi?