Muhubiri 5:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
5 Angalia kinywa chako kisikuingize katika zambi, halafu ikupase kumwambia mujumbe wa Mungu kwamba haukukusudia kutenda zambi. Kwa nini kumusukuma Mungu akukasirikie na kuiharibu kazi yako?
Ni kazi ya makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu kusudi watu wawaendee kwa kujifunza mapenzi yangu kwao, maana makuhani ni wajumbe wa Yawe wa majeshi.
Mbele haujauzisha lile shamba, si lilikuwa mali yako? Na nyuma ya kuliuzisha, feza ulizopata haungezitumia sawa unavyotaka? Basi namna gani ulikusudia kufanya jambo kama hili? Haukusema uongo mbele ya watu, lakini mbele ya Mungu!”
Unaweza kuomba faida unapomukopesha mugeni, lakini ndugu yako Mwisraeli usimulipishe faida, naye Yawe, Mungu wako, atakubariki katika shuguli zako zote utakazofanya katika inchi ambayo unakwenda kurizi.