Muhubiri 2:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
21 Maana, wakati mwingine, mutu ambaye amefanya kazi kwa kutumia hekima, akili na maarifa yake, anamwachia mutu mwingine afurahie matunda ya kazi ambayo hakuitoshea jasho. Hayo nayo ni bure. Ni jambo baya sana.
Pasaka kama hiyo ilikuwa haikufanyika katika Israeli yote tangu siku za nabii Samweli. Hakujatokea mufalme hata mumoja wa Israeli aliyefanya Pasaka kama hii iliyofanyika na mufalme Yosia, makuhani, Walawi na watu wote wa inchi ya Yuda, wa Israeli vilevile na wakaaji wa Yerusalema.
Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.
Unazani umekuwa mufalme kwa kujenga na mierezi? Baba yako alikula na kunywa, alifuata sheria yangu na kutenda mambo ya haki, na mambo yake yaliendeka vizuri.
Lakini macho yako wewe na moyo wako, vinaelekea tu mapato yasiyokuwa ya haki. Unamwanga damu ya wasiokuwa na kosa, nawe unawatesa watu na kuwatendea kwa ukali.