Na katika maono yale, nikaona wale farasi pamoja na wale waaskari waliopanda juu yao. Waaskari wale walikuwa na ngao zenye rangi nyekundu kama moto na zingine za rangi ya samawi na ya kimanjano kama kiberiti. Vichwa vya farasi wale vilikuwa kama vichwa vya simba, na ndani ya vinywa vyao mulitoka moto, moshi na mawe ya viberiti.