Biblia Todo Logo
線上聖經

- 廣告 -




Danieli 9:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Na sasa ee Bwana, Mungu wetu, uliyewaondoa watu wako katika inchi ya Misri kwa nguvu yako kubwa na kulifanya jina lako litukuzwe mpaka sasa, tunasema kwamba tumetenda zambi; tumefanya maovu.

參見章節 複製




Danieli 9:15
30 交叉參考  

Ulifanya miujiza na maajabu mbele ya Mufalme wa Misri, watumishi wake wote na watu wote wa inchi yake; maana ulijua kwamba waliwagandamiza babu zetu. Ukajipatia utukufu unaokuwa mpaka leo.


Tumetenda zambi, tumekosa, tumetenda maovu na kukuasi. Tumevunja amri zako na maagizo yako.


Watu wa Israeli ni watumishi wako na watu wako uliwakomboa kwa uwezo wako na mukono wako wenye nguvu.


Lakini Musa akamusihi Yawe, Mungu wake, akisema: Ee Yawe, kwa nini hasira yako inawaka vikali juu ya watu wako uliowatoa katika inchi ya Misri kwa uwezo mukubwa na mukono wenye nguvu?


Hakika, nitatukuzwa kwa kumwangamiza mufalme na jeshi lake, pamoja na magari yake na wapanda-farasi. Nao Wamisri watajua kwamba mimi ni Yawe.”


Lakini Yawe akamujibu Musa: “Sasa utaona jinsi nitakavyomutendea mufalme wa Misri. Kwa nguvu atalazimishwa kuwaacha watu wangu watoke. Kwa nguvu atawafukuza waondoke katika inchi yake.”


Yeye ndiye aliyetuopoa toka hatari kubwa sana ya kufa, naye atatuopoa tena. Nasi tunamutumainia kwamba ataendelea kutuopoa,


Lakini yule mulipishaji wa kodi alisimama kwa mbali, naye hakusubutu hata kuinua macho yake kuelekea mbingu; lakini alijipigapiga kwa huzuni na kusema: ‘Ee Mungu, unisamehe mimi mutenda mabaya.’ ”


Mwana wake akamwambia: ‘Baba, nimemukosea Mungu na nimekukosea wewe vilevile. Sababu hii sistahili kuhesabiwa tena sawa vile mwana wako.’


Nikatia sahihi juu ya barua ya ununuzi, nikaipiga muhuri, nikawaita washuhuda na kuipima ile feza juu ya mizani.


Pahali pa miiba kutaota miti ya shindano, na pahali pa michongoma kutaota misunobari. Hilo litakuwa jambo litakalowakumbusha watu juu ya mambo niliyotenda mimi Yawe, kitambulisho cha milele ambacho hakitafutwa.


Hata hivyo Mungu aliwaokoa kama alivyoahidi, kusudi aonyeshe nguvu yake kubwa.


maana ni watu wako, na ni mali yako, watu ambao uliwatoa Misri kutoka katika furu ya chuma.


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Kwa hiyo, uwaambie Waisraeli hivi: ‘Mimi ni Yawe! Mimi nitawatoa katika nira mulizowekewa na Wamisri. Nitawaokoa toka utumwa wenu. Nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuwaazibu vikali Wamisri na kuwakomboa ninyi.


Usisahau kwamba wewe ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri, nami Yawe, Mungu wako, nikakutoa huko kwa mukono wenye nguvu na mukono ulionyooshwa. Ndiyo maana mimi Yawe, Mungu wako, nimekuamuru kushika siku ya Sabato.


Musa akawaambia watu: “Mukumbuke siku hii muliyotoka inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa. Hii ndiyo siku Yawe alipowatoa humo kwa mukono wake wenye nguvu. Katika siku hii, musikule mukate uliotiwa chachu.


Na mambo haya yatakuwa ukumbusho, kama vile kitambulisho katika mikono yenu au katika paji la nyuso zenu; kusudi kiwakumbushe siku zote sheria ya Yawe. Maana, Yawe amewatoa katika inchi ya Misri kwa mukono wenye nguvu.


Kama kisha mwana wako akiuliza maana ya jambo hili, utamwambia: ‘Kwa nguvu ya mukono wake, Yawe alitutoa katika inchi ya Misri ambako tulikuwa watumwa.


Jambo hili litakuwa kama kitambulisho katika mukono wako au utepe katika paji la uso wako, kwamba Yawe alitutoa katika inchi ya Misri kwa mukono wenye nguvu.”


Nitawatendea hayo yote kwa sababu wameniasi na kunikasirikisha tangia wakati wazee wao walipotoka Misri mpaka leo.”


kama watakapokuwa kule katika uhamisho watajifikiri kwa roho yao yote na kwa moyo wao wote na kutubu na kukuomba musamaha, wakisema: ‘Tumetenda zambi; tumepotoka na kufanya maovu’,


Usikilize kwa uangalifu maombi yangu, na uniangalie mimi mutumishi wako, ninapokuomba kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli, usiku na muchana. Ninaungama zambi za watu wa Israeli, tulizofanya mbele yako. Mimi pamoja na watu wa jamaa yangu tumefanya zambi.


Wewe unakuja kuwasaidia wanaotenda haki kwa furaha, wanaokukumbuka na kufuata njia zako. Ulitukasirikia tulipokuwa wenye zambi; sisi tumeasi kwa muda murefu.


Tunakubali uovu wetu, ee Yawe, tunakubali uovu wa babu zetu, maana, tumekukosea wewe.


Tulikukosea na kukuasi, nawe haujatusamehe bado.


Lakini wakaaji wake wameyaasi maagizo na masharti yangu, wakakuwa wabaya kuliko mataifa na inchi zinazowazunguka. Kweli, wameyakataa maagizo yangu na kuacha kuyafuata masharti yangu.


跟著我們:

廣告


廣告