Danieli 5:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
17 Danieli akamujibu mufalme Belsasari: Unaweza kubakia na zawadi zako, ee mufalme, au kumupa mutu mwingine. Hata hivyo, ee mufalme, nitakusomea maandiko hayo na kukuelezea maana yake.
Elisha akamwuliza mufalme wa Israeli: “Kuna maneno gani kati yako nami? Kwenda uombe shauri kwa manabii ambao baba yako na mama yako waliwaendea.” Mufalme wa Israeli akajibu: “Sivyo! Yawe ndiye aliyetuita sisi wafalme watatu kusudi atutie katika mikono ya mufalme wa Moabu.”
Lakini Elisha akamwambia: “Unafikiri roho yangu haikukuwa pamoja nawe wakati mutu yule alipotoka ndani ya gari lake na kuja kukutana nawe? Huu ndio wakati wa kupokea feza na nguo, mashamba ya mizeituni na mizabibu, kondoo na ngombe au watumishi na wajakazi?
Pale pale, mufalme Belsasari akaamuru kwamba Danieli avalishwe nguo nzuri nyekundu na mukufu wa zahabu katika shingo. Ikatangazwa kwamba Danieli atakamata sasa nafasi ya tatu katika ufalme.