Danieli 4:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
11 Akalalamika kwa sauti akisema: Mukate muti huu na kuyakatakata matawi yake. Muangushe majani yake na kuyatawanya matunda yake. Nyama wakimbie toka chini yake na ndege kutoka matawi yake.
Watu wa mataifa mengine ya hatari sana, wataukata na kuuangusha chini na kuulalisha chini. Matawi yake yataanguka chini kwenye mulima na kila pahali katika mabonde; yatavunjika na kulala chini katika mitelemuko yote. Watu wote wataondoka chini ya kivuli chake na kuuacha.
Nawe, muji Kapernaumu, unafikiri kwamba utapandishwa mpaka juu mbinguni? Utashushwa mpaka chini katika kuzimu. Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yako ingalifanyika katika Sodoma, muji ule ungekuwa ungali hata leo.
“Musikilize enyi Waisraeli! Hivi leo mumekaribia kuvuka muto Yordani, kwenda kurizi inchi ya mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi. Miji yao ni mikubwa na ina kuta zinazofika katika mawingu.