Biblia Todo Logo
線上聖經

- 廣告 -




Danieli 2:46 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

46 Halafu mufalme Nebukadneza akaanguka uso mpaka chini na kumutukuza Danieli na kuamuru wamutolee Danieli sadaka na ubani.

參見章節 複製




Danieli 2:46
12 交叉參考  

Naye kuhani wa hekalu la mungu Zeu, lililokuwa kwenye kiingilio cha muji, akaleta ngombe waliopambwa na mafungu za maua mbele ya mulango. Maana yeye pamoja na kundi la watu walitaka kuwatolea wale mitume sadaka ya nyama wenye kuchinjwa.


Petro alipokuwa akiingia ndani ya nyumba, Kornelio akaenda kumupokea, akapiga magoti mbele yake na kumwabudu.


Haya yote yatatendeka kusudi waweze kumutolea Mungu wa mbinguni sadaka zinazomupendeza na waombee maisha yangu mimi mufalme na watoto wangu.


Ni mimi Yoane niliyesikia na kuona mambo hayo. Na wakati nilipokwisha kuyasikia na kuyaona, nilianguka mbele ya malaika aliyeyaonyesha kwangu kwa kumwabudu.


Nikaanguka mbele yake kusudi nimwabudu, lakini akaniambia: “Angalia, usifanye vile! Kwa maana mimi ni mutumishi kama vile wewe na wandugu zako wanaoshika ukweli ulioshuhudiwa na Yesu. Ni Mungu ndiye unayepaswa kumwabudu! Maana ukweli ambao Yesu alishuhudia, ndio uwezo unaowaongoza manabii.”


Miji yenu nitaiteketeza, pahali penu patakatifu nitapafanya jangwa na harufu zenu nzuri za sadaka sitazikubali.


Na wale wazee makumi mbili na wane wanaokaa juu ya viti vyao vya kifalme mbele ya Mungu, wakainama uso mpaka chini wakimwabudu Mungu,


Nao watu wale walingojea kuona ikiwa atavimba mukono au ataanguka mara moja na kufa. Lakini kisha kungoja muda murefu na kuona kwamba hakupata hasara yoyote, wakabadilisha mawazo yao hata wakasema kwamba yeye ni mumoja wa miungu.


Akainama uso mpaka chini mbele ya Yesu na kumushukuru. Mutu huyo alikuwa Musamaria.


mukisikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, munapaswa kuinama chini na kuabudu sanamu ya zahabu mufalme Nebukadneza aliyosimamisha.


Kwa hiyo, watu wote, mara tu waliposikia sauti za baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, walianguka uso mpaka chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu ambayo mufalme Nebukadneza alisimamisha.


Gabrieli akakuja karibu na pahali niliposimama. Mimi nikaogopa sana, hata nikaanguka uso mpaka chini. Lakini akaniambia: Wewe mutu, uelewe kwamba maono uliyoyaona yanaelekea wakati wa mwisho.


跟著我們:

廣告


廣告