Danieli 2:43 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
43 Hii ina maana kwamba watawala wa ufalme huo watachanganyikana kwa kuoana na watu wasiokuwa wa taifa lao, lakini hawatafikia kuchanganyikana kama vile chuma kisivyoweza kuchanganyikana na udongo wa mufinyanzi.
Kama ulivyoona, vidole vyake vya miguu vilikuwa nusu chuma na nusu udongo wa mufinyanzi, na hii ina maana kwamba ufalme ule utakuwa na sehemu moja yenye nguvu na sehemu ingine yenye uzaifu.
Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.