Danieli 11:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
8 Atabeba sanamu za miungu yao na vyombo vya bei kali vya feza na zahabu mpaka katika inchi ya Misri. Kwa muda wa miaka michache, mufalme wa kusini hatamushambulia mufalme wa kaskazini.
Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, alisema: Mimi nitamwazibu Amoni mungu wa muji wa Tebesi, nitaiazibu Misri na miungu yake na wafalme wake, nitamwazibu Mufalme wa Misri na wote wanaomutegemea.
Hata kama Efuraimu atastawi kama nyasi, mimi Yawe nitavumisha upepo mukali wa mashariki, upepo utakaotokea kule katika jangwa, nao utakausha visima vyake, chemichemi zake zitakauka. Vitu vyake vyote vya bei kali vitaharibiwa.
Muvunje mazabahu zao, na kubomoa kabisa nguzo zao. Muteketeze kwa moto sanamu zao za Ashera na kukatakata sanamu zao za kuchonga na kufuta kabisa jina lao na pahali hapo.
Mika akasema: “Ninyi mumebeba miungu yangu niliyojitengenezea, mukamutwaa na kuhani wangu, mukaniacha bila kitu chochote. Munaweza namna gani basi kuniuliza nina shida gani?”