Danieli 10:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
20 Naye akaniambia: Unajua kwa nini nimekuja kwako? Sasa ninapaswa kurudi kwenda kupigana na malaika mulinzi wa Persia. Halafu, nitakapokuwa nimemushinda, malaika mulinzi wa mufalme wa Ugriki atatokea.
Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.
Mukubwa wa ufalme wa Persia alinipinga kwa muda wa siku makumi mbili na moja. Lakini Mikaeli, mumoja kati ya wakubwa, akakuja kunisaidia, kwa hiyo nikamwacha kule pamoja na mukubwa wa ufalme wa Persia,
Nyuma ya mambo hayo, nikaona nyama mwingine. Huyu alikuwa kama chui mwenye mabawa mane ya ndege juu ya mugongo wake. Alikuwa na vichwa vine naye alipewa uwezo wa kutawala.
Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.