Ulipoanza kuomba, Mungu alitoa jibu, nami nimekuja kukuelezea jibu hilo kwa sababu unapendwa sana. Kwa hiyo, usikilize kwa uangalifu jibu hilo na kuelewa maono hayo.
Hata hivyo, ujipe moyo, ewe Zerubabeli. –Ni ujumbe wa Yawe. Ujipe moyo, Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki. Mujipe moyo nanyi watu wote wa inchi hii. –Ni ujumbe wa Yawe! Mufanye kazi, maana mimi niko pamoja nanyi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!
Enyi watu wa Yuda na watu wa Israeli! Wakati uliopita ninyi mulionekana kuwa watu waliolaaniwa kati ya watu wa mataifa. Lakini sasa mimi nitawaokoa, nanyi mutakuwa watu waliobarikiwa. Basi, musiogope tena, lakini mujipe moyo!
Yawe wa majeshi anasema hivi: Mujipe moyo! Sasa munayasikia maneno ambayo mulitangaziwa na manabii wakati musingi wa hekalu langu ulipowekwa kulijenga upya.
Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”
Petro akageuka, akaona nyuma yao mwanafunzi yule aliyependwa na Yesu. (Ni yeye aliyeegamia kifua cha Yesu wakati wa chakula na kumwuliza: “Bwana, ni nani yule atakayekutoa?”)
Lakini akanijibu: “Neema yangu inakutoshelea, kwa maana uwezo wangu unatimizwa katika uzaifu.” Basi tafazali nijivunie sana uzaifu wangu kusudi nijazwe na uwezo wa Kristo.
Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”
Wakati nilipomwona, nikaanguka chini kwa rafla mbele yake kama vile mufu. Lakini akaweka mukono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.