2 Samweli 8:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
6 Halafu Daudi aliweka kambi za waaskari katika muji wa Waaramu wa Damasiki. Basi, Waaramu wakakuwa watumishi wake na wakakuwa wanamulipa kodi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.
Kisha wafalme wote waliokuwa watumishi wa Hadadezeri walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli, walifanya mapatano ya amani na Israeli, nao wakakuwa watumishi wa Israeli. Hivyo Waaramu hawakusubutu kuwasaidia Waamoni tena.
Sasa, mulilete jambo hilo mbele ya watu kwa sababu Yawe alimwahidi Daudi hivi: ‘Kwa mukono wako wewe Daudi mutumishi wangu, nitawaokoa watu wangu Waisraeli kutoka Wafilistini na kutoka waadui zao wengine.’ ”
Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye utukufu kama wakubwa wengine katika dunia.
Kisha aliwashinda Wamoabu. Aliwapanga katika mistari mateka hao, na kuwalalisha chini. Aliamuru wale waliokuwa katika mistari miwili wauawe na wale wa mustari wa tatu waachwe wazima. Hivyo, Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakakuwa wanamulipa kodi.
Mambo mengine ya Yeroboamu, yote aliyofanya, vita alivyopigana kwa ushujaa, na jinsi alivyoikomboa Damasiki na Hamati na kuifanya mali ya Israeli, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
Mufalme Mesha wa Moabu alikuwa mufugaji wa kondoo, na kila mwaka alilipa kodi kwa mufalme wa Israeli wana-kondoo elfu mia moja na manyoya ya kondoo wengine elfu mia moja.
Aliweka majeshi katika miji yote ya inchi ya Yuda yenye kuta, na katika maeneo mengine ya Yuda akaweka waaskari walinzi, na katika miji ya Efuraimu ambayo baba yake Asa aliiteka.
Yonatani alishinda kambi ya waaskari ya Wafilistini kule Geba, na Wafilistini wote walisikia juu ya habari hiyo. Hivyo Saulo alipiga baragumu katika inchi yote, akatangaza, akisema: “Waebrania wasikie.”
Siku moja, Yonatani mwana wa mufalme Saulo alimwambia kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende ngambo kwenye kambi ya Wafilistini.” Lakini Yonatani hakumwambia baba yake.
Kulikuwa hofu kubwa katika kambi ya Wafilistini. Wote walianza kufazaika: waaskari katika kambi, watu katika mashamba kwenye kambi, hata na washambulizi. Inchi ilitetemeka. Hofu ilikuwa kubwa sana.
Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”