Biblia Todo Logo
線上聖經

- 廣告 -




2 Samweli 8:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 ni kusema Aramu, Moabu, Amoni, Filistini, Amaleki. Aliteka vilevile vitu vya mufalme Hadadezeri mwana wa Rehobu mufalme wa Zoba.

參見章節 複製




2 Samweli 8:12
10 交叉參考  

Waamoni walipoona kwamba Waaramu wamekimbia, nao vilevile walimukimbia Abisayi na kuingia katika muji. Yoabu akaacha kupigana na Waamoni, akarudi Yerusalema.


Zawadi zile, mufalme Daudi alizitakasa kwa ajili ya Yawe pamoja na feza na zahabu aliyonyanganya kwa mataifa yote, kutoka kwa: Waedomu, Wamoabu, Waamoni, Wafilistini na Waamaleki.


Kisha aliwashinda Wamoabu. Aliwapanga katika mistari mateka hao, na kuwalalisha chini. Aliamuru wale waliokuwa katika mistari miwili wauawe na wale wa mustari wa tatu waachwe wazima. Hivyo, Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakakuwa wanamulipa kodi.


Yoabu akamwambia Abisayi: “Ikiwa Waaramu wananishinda nguvu, utanisaidia lakini kama Waamoni wanakushinda nguvu, nitakuja kukusaidia.


Vilevile Daudi aliteka makundi yote ya kondoo na ngombe, na watu walioongoza nyama wale walisema: “Hivi ni vitu vya Daudi.”


Katika muda huo, Daudi na watu wake waliwashambulia Wagesuri, Wagirzi na Waamaleki, ambao walikuwa wenyeji wa inchi hiyo tangu zamani. Aliwashambulia katika inchi yao mpaka Suri, hata kwa mupaka na Misri.


Alimukamata mateka mufalme Agagi wa Waamaleki akiwa angali muzima. Akawaua watu kwa makali ya upanga.


Daudi aliwapiga tangu asubui mpaka siku ya pili magaribi. Hakuna mwanaume yeyote aliyeponyoka isipokuwa vijana mia ine ambao walipanda juu ya ngamia na kukimbia.


跟著我們:

廣告


廣告