2 Samweli 7:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye utukufu kama wakubwa wengine katika dunia.
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi. Ni ujumbe wa Daudi mwana wa Yese, ujumbe wa mutu ambaye Mungu alimufanya akuwe mukubwa, muchaguliwa wa Mungu wa Yakobo, mwimbaji muzuri wa zaburi wa Israeli:
Halafu Daudi aliweka kambi za waaskari katika muji wa Waaramu wa Damasiki. Basi, Waaramu wakakuwa watumishi wake na wakakuwa wanamulipa kodi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.
Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye heshima kama vile wakubwa wengine wa dunia.
Waaskari wa Wafilistini walikwenda kupigana na Waisraeli, lakini kila mara walipopigana vita, Daudi alipata ushindi kuliko watumishi wa Saulo. Hivyo jina la Daudi likazidi kusifiwa sana.
Anawainua wazaifu toka katika mavumbi, anawanyanyua wakosefu toka katika majivu, na kuwaikalisha pamoja na wakubwa, na kuwarizisha viti vya heshima. Maana, minara ya dunia ni ya Yawe; yeye ameisimika dunia juu ya minara yake.
Hivyo, wakalipeleka Sanduku hilo la Mungu kwenye muji wa Ekuroni. Lakini Sanduku hilo la Mungu lilipofika kule, watu wa muji huo walipiga kelele: “Wametuletea Sanduku la Mungu wa Israeli kwa kutuua sisi na watu wetu.”