1 Samweli 9:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
6 Yule mutumishi akamwambia: “Ngoja kidogo. Katika muji huu kuna mutu wa Mungu ambaye anaheshimiwa sana. Kila neno analosema linakuwa kweli. Sasa tumwendee. Labda anaweza kutuambia jinsi safari yetu itakavyokuwa.”
“Leo nilipofika kwenye kisima nikaomba: ‘Ee Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ninakuomba unisaidie leo katika safari yangu na umutendee Abrahamu bwana wangu mema.
Elisha, nabii wa Mungu, alipopata habari kwamba mufalme wa Israeli amepasua nguo zake, alituma ujumbe kwa mufalme, akamwuliza: “Kwa sababu gani umepasua nguo zako? Umutume mutu huyo kwangu, kusudi apate kujua kwamba kuna nabii katika Israeli!”
Lakini ninahakikisha ujumbe wa mutumishi wangu, na kukamilisha mipango ya wajumbe wangu. Mimi ndiye ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema, watu watakaa ndani yako tena. Na juu ya miji ya Yuda: Ninyi mutajengwa tena: mabomoko yenu yatatengenezwa tena.
Siku moja, mutu wa Yawe alimwendea Eli, akamwambia: “Yawe amesema hivi: Nilijijulisha kwa jamaa ya Haruni, babu yako, walipokuwa watumwa wa mufalme wa Misri katika inchi ya Misri.