Waaskari wengine wa kabila la Manase, wakatoroka na kwenda kujiunga na Daudi, wakati alipoondoka pamoja na Wafilistini kwenda kupigana na mufalme Saulo. (Lakini hata hivyo, hakuwasaidia maana watawala wa Wafilistini walifanya shauri wamufukuze arudie Ziklagi wakisema: “Tutahatarisa maisha yetu kwa sababu atatutoroka na kurudia kwa bwana wake Saulo.”)
Lakini wakubwa wa Wafilistini walimukasirikia sana Akisi, wakamwambia: “Umurudishe aende pahali ulipomupa akae. Asiende hata kidogo pamoja nasi kwa vita, kama sivyo wakati wa vita atageuka na kuwa adui yetu. Hauoni kwamba mutu huyu atapata njia nzuri ya kupatana na bwana wake halafu kuwa adui yetu katika vita?