1 Samweli 27:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
10 Akisi alipomwuliza: “Leo mashambulizi yako yalikuwa juu ya nani?” Daudi alimwambia: “Juu ya Negebu ya Yuda” au “Juu ya Negebu ya Wayerameli” au “Juu ya Negebu ya Wakeni”.
Watumishi wa Abusaloma walipofika kwa yule mwanamuke, wakamwambia: “Ahimasi na Yonatani wako wapi?” Yule mwanamuke akawaambia: “Wamekwenda ngambo ya kijito.” Walipowatafuta na kuwakosa, wakarudi Yerusalema.
Wazao wa Keni ambaye alikuwa baba mukwe wa Musa, walifuatana na watu wa kabila la Yuda kutokea Muji wa Miti ya Ngazi, ni kusema muji wa Yeriko, mpaka jangwa la Yuda karibu na Aradi, wakafanya makao yao kule pamoja na watu wa Yuda.
Wakati ule, Mukeni mumoja aliyeitwa Heberi alikuwa amejitenga na Wakeni wenzake ambao ni wazao wa Hobabu, baba mukwe wa Musa. Alikuwa amepiga hema lake mbali kule kwenye muti wa mwalo wa Sananimu, karibu na Kedesi.
Saulo akawaambia Wakeni: “Muende! Muondoke! Mutoke kati ya Waamaleki, kama sivyo, nitawaangamiza pamoja nao. Muondoke kwa sababu ninyi muliwatendea mema Waisraeli walipotoka Misri.” Basi, Wakeni wakaondoka kati ya Waamaleki.
Daudi hakumwacha mutu yeyote muzima akuwe mwanaume au mwanamuke kusudi aletwe Gati; alifikiri ndani ya moyo: “Wanaweza kueleza juu yetu na kusema: ‘Daudi alifanya kitendo hiki na kile.’ ” Hivyo ndivyo Daudi alivyozoea kutenda wakati wote alipoishi katika inchi ya Wafilistini.
Daudi akamwambia Akisi: “Lakini nimefanya nini? Kama unavyosema kwamba haujaniona na kosa lolote tangu siku ile nilipoanza kukutumikia mpaka leo, kwa nini nisiende kupigana na waadui za bwana wangu mufalme?”